Mjukuu apanga mauaji ya babu yake kwa milioni moja

Date:

Share post:


RUKWA

Mzee mwenye umri wa miaka 72 aliyefahamika kwa jina la Paul Kisiwa, ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Ng’ongo ameawa kwa kupigwa rungu kichwani.
Mzee huyo aliuawa Machi 3, mwaka huu majira ya jioni katika Kijiji cha Kifinga kilicho Kata ya Mtowisa wilayani Sumbawanga.
Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando ambaye amesema watu sita akiwemo mjukuu wa mzee huyo wanashikiliwa na polisi.
Kamanda Kyando alisema mjuu wa mzee Kisiwa alikubali kuchukua sh. Milioni moja ili babu yake auawe.
Diwani wa Kata ya Mtowisa, Edger Malinyi naye amekaririwa akieleza kuwa mzee huyo ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kata wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) alizikwa kimya kimya shambani kwake baada ya kuuawa.
“Taarifa za kupotea kwa Kisiwa zilianza kuzagaa. Ndugu na jirani zake wakishirikiana na polisi walianza kumtafuta, ilipofika Machi 8, mwaka huu walimbana mjukuu wake ambaye alikiri kupanga njama za kumuua babu yake baada ya kupewa Sh. 1,000,000.“Alipobanwa alieleza kuwa alipanga njama ya mauaji hayo na watu waliokuwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu na babu yake.
“Kwamba babu yake aliwakodishia watu hao shamba la ekari zaidi 15 kwa ajili ya shughuli za kilimo lakini baadaye aliwanyang’anya akaanza kulilima mwenyewe ndiyo wakakasirika wakaandaa mpango wa kumuua.
“Siku ya tukio la mauaji walimvamia akiwa shambani kwake, wakampiga na rungu kichwani ambalo lilimuua papo hapo.
“Baada ya kumuua, walichimba shimo shambani humo wakamzika ili kupoteza ushahidi. Mjukuu wake alionyesha mahali alipozikwa na polisi walipofukua waliukuta mwili wa mzee huyo,” alisema diwani huyo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...