OCEAN ROAD WATIBU KWA MIONZI YA NYUKLIA

Date:

Share post:

Ocean Road


DAR ES SALAAM
TAASISI ya Saratani ya Ocean Road inatibu watu zaidi 2000 kila mwaka kwa kutumia mionzi ya Nyuklia.Hayo yameelezwa leo na Daktari Bingwa na Mtaalamu wa Uchunguzi na Tiba ya Mionzi wa taasisi hiyo, Tausi Maftah.
Maftah aliisifu teknolojia hiyo kwa kueleza kuwa ni ya hali ya juu katika uchunguzi na tiba dhidi ya magonjwa mbalimbali.
Alisema ingawa Ocean Road ni taasisi ya saratani lakini kwa kutumia teknolojia hiyo ina uwezo wa kuchunguza na kutibu magonjwa mengine yakiwamo ya moyo na figo.
Alisema huduma hiyo imeanzishwa pia katika Hospitali ya Bugando mkoani Mwanza.
Dk. Maftah alisema Ocean Road inaagiza mionzi ya Nyuklia kutoka Afrika Kusini na Bugando inaagiza kutoka Uturuki.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

GUARDIOLA AMPONZA KOCHA WA BURNLEY

LONDON, Uingereza KOCHA wa Burnley, Scott Parker, amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Manchester...

BERNARDO AWEKA REKODI MPYA MAN CITY

MANCHESTER, Uingereza KATIKA ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley, kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, ameweka rekodi ya...

MABOSI WAMTAKA BRUNO KUBAKI UNITED

MANCHESTER, Uingereza UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno,...

CESC FABREGAS KOCHA MPYA CHELSEA?

LONDON, Uingereza KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania,...