KENYA YAONDOA SHARTI LA USAFIRI WA ANGA KWA TANZANIA

Date:

Share post:

 

NA CHARLES MULLINDA

MAMLAKA ya Usafiri wa Anga ya Kenya (KCAA) imeondoa sharti la kuwekwa karantini kwa siku 14 kwa wasafiri wa ndege wanaoingia nchini humo wanaotokea Tanzania.

Taarifa ya kuondolewa kwa sharti hilo imetolewa Septemba 16 na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyoeleza kuwa KCAA iliondoa sharti hilo Septemba 15.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Serikali ya Tanzania nayo imeondoa amri ya kuzuia kampuni za ndege za Kenya kufanya safari zake nchini Tanzania.

“Kufuatia hatua hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeondoa amri ya kuzuia kampuni za ndege za Kenya ikiwemo Kenya Airways, Fly 540 Limited, Safarilink Aviation na AirKenya Express Limited kufanya safari zake nchini Tanzania.

” Kwa taarifa hii, sasa kampuni hizo za ndege za Kenya zimeruhusiwa kurejesha safari zake nchini mara moja na tayari Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Kenya imejulishwa kuhusu uamuzi huo,” ilieleza taarifa hiyo.

Aidha, katika taarifa yake hiyo, Johari ilieleza  kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuendesha na kusimamia shughuli za usafiri wa anga kwa kuzingatia misingi ya kimataifa ya usafiri wa anga kama ilivyoainishwa katika mkataba wa Chicago wa mwaka 1944 na mkataba wa usafiri wa anga baina ya nchi na nchi.

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

DUTERTE KUPANDISHWA KIZIMBANI ICC

MANILA, Ufilipino JOPO la majaji watatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) limethibitisha kuwa Rais wa zamani wa...

WRIGHT: RICE APEWE BALLON D’OR

LONDON, Uingereza MKONGWE wa Arsenal, Ian Wright, amemtaja Declan Rice kuwa anastahili kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka...

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...

RAIS RAMAPHOSA ‘AMTUMBUA’ MKUU WA POLISI

PRETORIA, Afrika Kusini RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie...