DC MURRO AMSHUKURU RAIS SAMIA KUMALIZA KERO YA MAJI IKUNGI

Date:

Share post:


RIPOTA PANORAMA

0711 46 49 84 

MKUU wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro ameweka jiwe la msingi katika mradi wa maji ya bomba wa rafiki Ikungi unaotarajiwa kuwanufaisha wakazi wa Kata za Unyahati na Ikungi

Murro aliweka jiwe hilo la msingi mapema mwezi huu ambapo thamani ya mradi ni Shilingi milioni 548 ambazo ni sehemu ya fedha za Uviko -19 

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi, Muro alisema mradi huo katika awamu ya kwanza utakuwa na maeneo nane ya umma ya kuchotea maji (vilula) na pia umetengenezwa ukiwa na uwezo wa kutoa huduma ya kuwaunganishia wananchi maji majumbani kutokana na miundombinu yake kupita kwenye maeneo ya makazi ya watu 

Muro alisema fedha tumika kujenga mradi huo ni sehemu ya fedha ambazo Rais Samia Suluhu Hassan alizitoa kwa Wilaya ya Ikungi ikiwa ni sehemu ya mapambano ya changamoto ya ugonjwa wa Uviko -19 na kwa sasa mradi umekamilika kwa asilimia 98 na vilula vyote vinatoa maji.

Alimshukuru Rais Samia kwa kuridhia Ikungi kupewa fedha hizo na kumuhakikisha kuwa zimesimamiwa kikamilifu mpaka mradi kukamilika na pia aliwapongeza watekelezaji wa mradi huo ambao ni Ruwasa Ikungi na Mkoa wa Singida.


About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...