SERIKALI, WASHIRIKA WA MAENDELEO KUREJESHA UHUSIANO

Date:

Share post:

BENNY MWAIPAJA, DODOMA

SERIKALI imekubaliana na washirika wa maendeleo kurejesha uhusiano wa karibu na wenye tija ili kusaidia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano na Mkakati wa Kukuza Uchumi Zanzibar (MKUZA III).

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa mazungumzo ya kimkakati baina ya Serikali na washirika wa maendeleo kutoka nchi mbalimbali duniani mjini Dodoma mapema wiki hii, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James alisema mwongozo wa ushirikiano wa maendeleo kati ya Serikali na washirika wa maendeleo una malengo mbalimbali.

Alisema mwongozo huo wa miaka saba, 2017/2018 hadi 2014/2025, umelenga kuipa Serikali nafasi ya kuongoza mchakato wa maendeleo na kuijengea Serikali uwezo wa kukusanya mapato ya ndani, kuchambua fursa muhimu za uwekezaji na kutumia masoko ya kikanda na kimataifa kupata faida.

Mratibu wa Umoja wa Mataifa na kiongozi wa washirika hao, Alvaro Rodriguez aliahidi kushirikiana na Tanzania ili malengo yake ya maendeleo yaweze kufikiwa kwa kuboresha ushirikiano uliokuwa umeanza kulegalega.

Serikali na washirika wa maendeleo walifikia makubaliano ya kukutana mara mbili kwa mwaka. Kikao kingine kinatarajiwa kufanyika Novemba, mwaka huu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...

NEWCASTLE KUMUUZA MSHAMBULIAJI WA BEI MBAYA

LONDON, UingerezaKLABU ya Newcastle United itampiga bei straika raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Yoane Wissa,...

LIVERPOOL NAYO YAJITOSA KWA WHARTON

MERSEYSIDE, UingerezaLIVERPOOL imeungana na klabu zingine kubwa za Ulaya zinazomtolea macho kiungo wa Crystal Palace, Adam Wharton. Mtandao wa...

SINTOFAHAMU KUELEKEA MAZUNGUMZO YA PILI KATI YA MAREKANI, IRAN

WASHINGTON DC, MarekaniAKIZUNGUMZA na waandishi wa habari Aprili 16, 2026, Rais wa Marekani, Donald Trump, alisema ana matumaini...