WAZIRI MKUU MAJALIWA ATAKA UDHIBITI MIMBA TANDAHIMBA

Date:

Share post:

RIPOTA WA WAZIRI MKUU

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametaka kuwepo udhibiti wa mimba za utotoni katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

Akizungumza jana na watumishi na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba, alisema ni lazima viongozi wasimamie nidhamu kwa kuwalinda watoto wa kike wa wilaya hiyo dhidi ya mimba ili waendelee na masomo.

“Kwa nini kila mwaka mimba Tandahimba zinaongezeka, viongozi simamieni utekelezaji wa sheria kwa kuwachukulia hatua wote waliowapa mimba wanafunzi.

“Lazima wahusika wote wakamatwe wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria kwa sababu wanaharibu elimu ya mtoto wa kike,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka wazazi na walezi wa watoto wenye mahitaji maalumu kutowafungia ndani na badala yake wawapeleke shule.

“Watakaobainika kuwafungia ndani watoto wenye mahitaji maalumu wachukuliwe hatua za kisheria kwa sababu wanawakosesha haki ya kupata elimu,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...