RUFAA YA SUGU YAKAMILIKA

Date:

Share post:

RIPOTA MAALUMU
MAWAKILI wa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) na Katibu wa Kanda ya Nyasa, Emmanueli Masonga wamekamilisha taratibu za ukataji wa rufaa ya kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya.

Mmoja wa mawakili wa Sugu, Faraji Mangula jana aliwaeleza waandishi wa habari mjini hapa kuwa tayari wameshakamilisha taratibu zote muhimu za kukata rufaa hiyo wanachosubiri ni kupangiwa tarehe na Mahakama Kuu.

Wakili Mangula alieleza kuwa anatumaini mahakama itapanga haraka tarehe ya kuanza kusikiliza kesi ya Sugu.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga walihukumiwa kifungo cha miezi mitano gerezani bila faini baada ya kukutwa na hatia ya kutamka maneno ya fedheha yaliyomlenga Rais Dk. John Magufuli kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Disemba 30, mwaka 2017 katika viwanja vya Shule ya Msingi ya Mwenge ya jijini Mbeya.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...