MATUKIO katika picha, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokutana na kusalimiana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Sechelela ya jijini Dodoma katika viwanja vya Bunge jana na pia akisalimiana na wabunge mbalimbali kabla ya kuingia kwenye kikao cha Bunge jana.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sechelela ya jijini Dodoma kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 30, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sechelela ya jijini Dodoma kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 30, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 30, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 30, 2023. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kulia), Mbunge wa Urambo, Margaret Sitta (wa pili kulia) na Mbunge Mpanda Vijijini, Selemani Kakoso kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 30, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)