Sunday, June 22, 2025
spot_img

SEREKALI YAPOTEZA MABILIONI NA HATARINI KUPOTEZA HISA ZA MECCO

 

Mfanyabiashara Abdulkadir Mohamedi    

RIPOTA PANORAMA
0711 46 49 84

UTATA umeibuka baada ya kubainika kwamba Serikali kupitia Msajili wa Hazina (TR) imekua ikipoteza fedha nyingi kutokana na hisa zake katika kampuni mbalimbali kutosimamiwa ipasavyo na nyingine kuchukuliwa kinyemela.

Tayari Serikali inatajwa kupoteza mamilioni ya Shilingi zinazopatikana kupitia hisa zake asilimia 25 ilizokuwa ikizimiliki katika Kampuni ya Mwananchi Engineering and Contracting Company Ltd (MECCO) kwa takriban miaka kumi sasa.

“Hadi sasa Serikali haijaambulia chochote kwenye fedha zaidi ya Shilingi bilioni tano ambazo zinatokana na biashara inayofanyika katika eneo la MECCO kutokana na mfanyabiashara mwenye hisa asilimia 75 kutowasilisha fedha hizo serikalini,” amesema mtoa habari wetu.

Taarifa zinaeleza kwamba eneo la MECCO ambalo lilipaswa kuwa la Serikai linamilikiwa na mfanyabiashara mwenye asili ya Kisomali, Abdulkadir Mohamedi ambaye anatajwa kuwa na hisa asilimia 75 ya hisa zote.

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kwamba baada ya kifo cha kigogo mmoja serikalini ambaye alikua anaiwakilisha Serikali (jina tunalihifadhi kwa sasa), mfanyabiashara huyo sasa ameamua kuchukua hata asilimia 25 ya hisa za Serikali.

Taarifa zinasema mfanyabiashara huyo ameshafanya mchakato wa kubadilisha umiliki na hata jina kutoka MECCO na kuwa MAS, akitaka kufanya biashara ya kuhifadhi na kusimamia makontena

Aidha, taarifa zaidi zinaeleza kuwa Mohamedi amehamishia hisa hizo za Serikali kwenye Kampuni yake ya MAS na kwamba baadhi ya watendaji wa Serikali ambao wamekuwa wakijaribu kuhoji kuhusu uhalali wa hisa za Serikali kuchukuliwa naye, amekuwa akiwatisha kwa kutumia majina ya baadhi ha viongozi wakubwa wa Serikali.

Mohamedi mwenyewe amekuwa kimya kila alipoulizwa kuhusu hilo na pia PANORAMA Blog imemtafuta bila mafanikio Msajili wa Hazina ili kuzungumzia suala hili lakini jitahada za kumpata zinaendelea.

Kampuni ya Mwananchi Engineering and Contracting Company Limited ni moja kati ya kampuni kubwa iliyoanzishwa zaidi ya miaka 50 iliyopita na imetekeleza miradi mingi mikubwa hapa nchini.

Baadhi ya miradi mikubwa iliyotekelezwa na MECCO ni pamoja na ujenzi wa jengo la Benki Kuu ya Tanzania lililopo Arusha na Hotel ya Mount Meru iliyopo Arusha pia. Mkoani Tanga MECCO imejenga Jengo la Hospitali ya Bombo na katika Mkoa wa Dar es Salaam imejenga Jengo la Makao Makuu ya Bima (NIC)

Miradi mingine iliyotekelezwa na MECCO katika Mkoa wa Dar es Salaam ni Ujenzi wa Soko la Kariakoo, Makao Makuu ya Kampuni ya Sigara pamoja na miradi mingine mingi ya ujenzi wa barabara, madaraja, barabara za kurukia ndege na mitalo ya maji.

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya