Sunday, June 29, 2025
spot_img

TUHUMA ZA RAVJI DHIDI YA MURTAZA DEWJI WA MeTL ZINA MIAKA MINNE

 

Rais Dk. John Magufuli

NA MWANDISHI WETU

‘TUHUMA za kughushi nyaraka na saini pamoja na malalamiko ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu (utapeli) zinazotolewa na Kampuni ya Ravji Construction Limited dhidi ya Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) zina zaidi ya miaka minne sasa.

Haya yanabainishwa na barua ya wazi kwa Rais Dk. John Magufuli ya Feruari 29, 2016 iliyosainiwa na K.J Uisso aliyejitambulisha kama raia mwema, aliyeandika akimuomba Rais msaada wa kutumbua jipu linalokwamisha kesi nambari WH/IR/2657/2014 ambayo mtuhumiwa ni Murtaza Dewji mwenye kosa la kughushi.

Barua hiyo yenye kichwa cha maneno, ‘barua ya wazi kwa Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Yah: malalamiko ya jalada la kesi Na. WH/IR/2657/2014. Mtuhumiwa: Murtaza s/o Dewji: kosa kughushi, inasomeka hivi;



‘Tafadhali husika na kichwa cha habari hapo juu.

‘Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tumelazimika kuandika barua hii ili kuleta malalamiko yetu kwako juu ya sintofahamu ya jalada la kesi husika, WH/IR/2657/2014, Murtaza s/o Dewji toka Wazo Hill Polisi Station, kughushi hati na saini.

‘Mheshimiwa Rais jalada hili lilipelekwa ofisi ya mwanasheria tangu tarehe 10/12/2014 lakini mpaka tunaandika barua hii shauri hili la jinai halijapelekwa mahakamani zaidi ya mtuhumiwa kutamba kuwa hakuna mtu wa kumfanya lolote kwani serikali ameiweka mfukoni.

‘Mnamo tarehe 27/01/2015, mwanasheria wa Kanda ya Dar es Salaam  aliomba apewe siku mbili ili apeleke kesi mahakamani. Baada ya kusubiri kama alivyotuelekeza mwanasheria wa kanda tukavuta subira mpaka tarehe 12/02/2015. Hakuna kilichoendelea tukalazimika kupeleka malalamiko yetu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa barua ambayo niliwasilisha malalamiko yangu rasmi Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kueleza jinsi nilivyocheleshwa haki yangu tangu nimefungua jalada la uchunguzi katika kituo cha polisi Wazo Hill, Mei 2014.

‘Ofisi ya DPP ilinijibu barua yangu tarehe 13/03/2014 yenye kumb, Na AGC/PP/C.110/54/29 ambayo walikiri kupokea na wanayafanyia kazi malalamiko yangu na ufumbuzi ukipatikana watanijulisha.

‘Terehe 23/04/2015 niliandikiwa barua nyingine na Mkurugenzi E. Kakolaki yente Kumb. Na. AGC/PP/c.110/54/37 na kueleza kubainika kwa mapungufu kwenye hilo jalada hivyo tarehe 15/02/2015 faili lilirudishwa polisi.

‘Tarehe 14/09/2015 niliandikiwa barua nyingine yenye Kumb. Na.ABC/PP/C.190/36104/17 kunijulisha kuwa kosa lenyewe ni kubwa hivyo ni vema upelelezi ukafanywa kwa umakini mkubwa na kwamba niedelee kuvuta subira. Iliandikwa na M. Mchungahela.

‘Mheshimiwa Rais baada ya kuona mwaka wa pili na nusu umeisha nikaona ni vema niwakumbushe tena kwa barua yangu ya tarehe 04/01/2016 Kumb. Na. RCL/Mbezi/Plot105/56 na kuwaeleza kuhusu haki yangu inavyocheleshwa kwani inaonekana inapotea. Nilijibiwa kwa barua ya terehe 28/10/2016 yenye Kumb. Na. ACG/PP/C190/3/04/21 ambayo inaeleza upelelezi unachukua muda mrefu kwa sababu unahusisha vyombo vingine zaidi ya Polisi na kwamba File liko kwa Mkurugnzo wa Makosa ya Jinai (DCI)

‘Mh. Rais mpaka hivi leo tunaandika barua hii hatujaona juhusi zozote za kufikisha suala hli mahakamani zaidi ya kuzungushwa na watendaji hasa wakurugenzi katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Divisheni ya Mashitaka.

‘Mheshimiwa Rais tunaomba ofisi yake itusaidie kutumbua hiki kijipu.’

Tanzania PANORAMA Blog inaendelea na uchunguzi wa sakata hili.

 

 

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya