Thursday, June 26, 2025
spot_img

POLISI DAR WAUA WATUHUMIWA WAWILI WA UJAMBAZI

 

IGP Simon Sirro

NA MWANDISHI WETU

JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni limewaua watu wawili wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio ya wizi toka maungoni, kuvunja nyumba na maduka usiku na kuiba, unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi wa pikipiki.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni (RPC), Kamishna Msaidizi, Ramadhani Kingai, imeeleza kuwa watuhumiwa hao wa uhalifu waliuawa wiki iliyopita katika eneo la Mbezi Luis wakati wakipambana kwa risasi na polisi wa kikosi maalumu cha kupambna na majambazi cha Mkoa wa Kinondoni.

Katika taarifa yake hiyo, RPC Kingai alieleza kuwa X.F. 407. CLP Bundala Said Kimenya na X.F. 1205 CLP  Muhidin Sadick Mhina, ambao ni askari waliofukuzwa jeshini kutokana na matendo yao kihalifu waliuawa baada ya kukurupushwa na polisi wakijiandaa kufanya tukio la kihalifu.

“Mnamo tarehe 26/11/2020 majira  ya saa 12 jioni  huko maeneo ya Kimara Luguruni, Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni lilikuwa na taarifa fiche kuwa kuna majambazi wamepanga kufanya uhalifu kwa kutumia silaha katika eneo la Kiluvya.

“Kikosi maalumu cha kupambana na majambazi Mkoa wa Kinondoni kiliweka mtego eneo la Luguruni eneo la Sheli iitwayo hapa kazi tu karibu na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, ambapo majambazi hayo yalikuwa yakitokea Kimara kulekea Kiluvya kupitia Morogoro Road.

“Walipofika eneo hilo wakiwa gari T 889 DKG, Toyota Brevis, rangi ya  Silver walisimamishwa na askari polisi lakini hawakusimama, waligeuza gari yao kwa kasi kurudi walikotoka, ndipo askari walipoanza kuwakimbiza majambazi hao ambao wakaanza kufyatua risasi hovyo.

“Walipofika eneo la Mbezi Luis karibu na Shule ya St Anne Pr & Sec School, askari walifanikiwa kupiga tairi risasi ambapo gari lilipoteza mwelekeo na kuingia mtarano, jambazi mmoja aliuawa pale pale na watatu walikimbia huku mmoja akiwa amejeruhiwa mguu,’ inasomeka sehemu ya taarifa ya RPC Kingai.

Aidha, inaendelea kuwa baadaye polisi wakiwa katika ufuatiliaji walijulishwa kuwepo kwa jambazi eneo la standi ya Kibo aliyekuwa akitaka kupanda gari huku akiwa amejeruhiwa mguu ambapo askari walifika haraka kumtia mbaroni akiwa na silaha.

Tatarifa inaeleza zaidi kuwa Mhina na Kimenya ni askari waliofukuzwa kazi kabla ya kuuawa kutokana na matendo yao ya kihalifu na kwamba watuhumiwa wengine wawili wanaendelea kutafutwa.

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila.

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya