Monday, June 23, 2025
spot_img

MWANAFUNZI ALIYEPOTEA ST MARY’S APATIKANA

Labna

 

NA MWANDISHI WETU

LABNA Salim Said,  mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Bweni ya St. Mary’s iliyopo Mbezi Makonde ambaye alipotea tangu Oktoba 4, 2020, amepatikana.

Mwanafunzi huyo alipatikana Disembe 12, 2020, eno la Banana Relini akiwa amewekwa kinyumba na mwanaume ambaye jina lake halikufahamika mara moja baada ya kufanikiwa kuwakimbia polisi waliokwenda kuwakamata.

Taarifa za kupatikana kwa Labna zilithibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni (RPC) Ramadhani Kingai katika mahojiano mafupi kwa njia ya simu ambaye alisema, taarifa za kupatikana kwa mwanafunzi huyo anazo lakini hawezi kuongea zaidi kwa sababu yupo kwenye kikao.

Mama mzazi wa Labna anayefahamika kwa jina la Rabia Swedan alisema walipata taarifa za kuwepo kwa mtoto wao eneo Banana Relini usiku na walifika eneo hilo wakiwa wameambatana na polisi wawili na kumkuta akiwa amelala chini pamoja na aliyemtorosha.

“Inasikitisha, tulipata taarifa za huyu mtoto kuwepo Banana Relini usiku, tukaenda Kituo cha Polisi Stakishari kuomba polisi, tukapewa wawili tukaambatana nao mpaka kwenye hiyo nyumba tukawakuta wamelala chini. Yule bwana aliyekuwa naye alipotuona na polisi akakurupuka akakimbia, sasa kwa sababu polisi walikuwa wawili hawakuweza kumfukuza.

“Mtoto alikuwa hoi, tulimpeleka Stakishari polisi huo usiku wa saa saba akakaa hapo wakimuhoji mpaka saa 12.00 asubuhi, kwa jinsi alivyokuwa wakatuambia tumpeleke hospitali.

“Tukampeleka Hospitali ya Amana na baada ya matibabu tukamchukua hadi Kituo cha Polisi Goba kwa sababu ndiko kesi yake inakopelelezwa, nao  wakamuhoji wakaturudishia tuendelee kumtibu ila akiwa na nafuu tutampeleka tena polisi,” alisema Swedan.  

Mwanafunzi msichana Labna wa Shule ya Sekondari ya Bweni ya St. Mary’s iliyoko Mbezi Makonde alitoweka shuleni tangu Oktoba 4, 2020 na kutokomea kusikojulikana hadi alipopatikana Disemba 12.

Labna alitoweka akiwa chini ya uangalizi wa shule lakini taarifa za kutoweka kwake zilitolewa Oktoba 8, 2020 na matron wake, Sarah Murra aliyempigia simu mama mzazi wa Labna akiulizia kama ameishafika nyumbani.

Katika hatua ya kushangaza, uongozi wa Shule ya Sekondari ya St Mary’s haukutoa taarifa polisi kuhusu kutoweka kwa mwanafunzi huyo na badala yake wazazi ndiyo walioripoti tukio la mtoto wao kupotea akiwa shuleni.

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya