Tuesday, June 24, 2025
spot_img

KAMANDA BUKOMBE AONDOLEWA KINONDONI, APELEKWA MAKAO MAKUU

 

Kamanda Bukombe

NA MWANDISHI WETU

ALIYEKUWA Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni (RPC), Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Edward Bukombe, amehamishwa kituo chake cha kazi na kupelekwa makao makuu.   

Taarifa zilizoifikia Tanzania PANORAMA Blog kutoka vyanzo vyake vya habari zimeeleza kuwa Kamanda Bukombe sasa anakwenda kuongoza kitengo cha picha na matukio na kwamba uhamisho huo ni wa kawaida.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, nafasi ya Kamanda Bukombe imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ramadhani Kingai ambaye katika mahojiano yake leo na Tanzania PANORAMA Blog amethibitisha kurithi wadhfa huo akitokea mkoani Arusha.  

 

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya